Irene Uwoya ‘Ni muda wa mwanaume mpya’

Baada ya tetesi kuenea kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na muigizaji Irene Uwoyapamoja na mume wake Dogo Janja kuwa wameachana ingawa wawili hao hawajaongea chochote kuhusiana na kuachana kwao.

Irene Uwoya ameonekana kuwa mbioni kutafuta mwanaume mwingine hii ni baada ya kuandika caption iliyoonyesha hivyo kupitia ukurasa wake wa Instagram na kusema hali ya hewa inamshawishi kufanya hivyo.

“Hewa ya nje niko tofauti siku ya leo, inanukia kama vile ni muda wa mwanaume mpya” >>>Irene Uwoya